Tuesday, 12 April 2011

KIMWANA MANYWELE TWANGA PEPETA 2011 YAWADIA

Kiongozi wa bendi ya African Stars International 'Twanga Pepeta' Luiza Mbutu (kushoto), akiongea jambo kwa wanahabari, kulia ni mratibu wa shindano hilo Maimartha Jesse.
Baadhi ya Waandi waHabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua kumbukumbu kwenye hafla hiyo.
Kimwana Manywele Twanga pepeta namba mbili 2007, Husna Idd 'Sajenti' akiongea jambo kwa waandishi wa habari.
Baadae Sajenti aliunda pozi namna hii.

SHINDANO la kumsaka Kimwana Manywele Twanga Pepeta 2011, limewadia ambapo warembo hao wataanza kuchuana rasmi mei 6 mwaka huu ndani ya ukumbi wa Sun Cirro Club,
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, mratibu wa shindano hilo, Maimartha Jesse, alisema kuwa mshindi atakaye patikana kwa mwaka huu atazawadiwa Duka la Vipodozi lenye thamani isiyopungua shilingi milioni tano, (5,000,000/=), ambalo pia litakuwa Wilaya ya Kinondoni.
Maimartha aliongeza kuwa, Duka hilo litalipiwa kodi na leseni ya mwaka mzima bila kuainisha jina la mmiliki maana atakuwa hajafahamika kwea wakati huo.

Warembo hao wanatalajiwa kuingia kambini kuanzia jumanne ijayo kwaajili ya mazoezi, ambayo watajifua chini ya kiongozi wa Wanenguaji wa Bendi hiyo Kassim Mohamed 'Super K'.

No comments: